Wednesday, December 28, 2011
Thursday, November 17, 2011
HAPPY BIRTHDAY MARTIN. ( 18 NOV )
Katika kuikumbuka siku yako ya kuzaliwa leo tunakutakia kila la kheri na Mungu akujalie maisha marefu yenye AMANI, UPENDO na kila aina ya FANAKA.
HAPPY BIRTHDAY MARTIN.
Wednesday, November 16, 2011
HAPPY BIRTHDAY MAMA ( 17 Nov )
Dear Mama. |
Mama hongera sana kwa kuifikia siku ya leo ambayo unakumbuka siku ya kuzaliwa kwako. Awali ya yote tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kukuzidishia kila lililo jema na hasa afya iliyo njema ya kukufikisha siku ya leo.Tunajivunia sana kuwa na wewe Mama kwani kwa pamoja na Baba mmeweza kutukuza katika malezi yaliyo bora na hata kututimizia kila lililo hitaji katika maisha yetu mpaka leo.Mungu awabariki na kuwazidishia na naamini kabisa kwa pale milipopungukiwa kwa kutuhangaikia wanenu Mungu atapajaza tu. Mama tunakushukuru sana kwa yote na tunazidi kukuombea kwa Mwenyezi Mungu akuzidishia siku kama hii ya leo nyingi tu huko mbeleni na naamini tutazidi tu kuikumbuka siku hii na kuiheshimu siku zote.Umetufunza mengi na umetukanya mengi ambayo leo hii tunajivunia na kuyatambua.Hakika hakuna kama Mama. Tunakupenda sana Mama na tunakuhitaji sana Mama hivyo tunaomba hata siku hii ya leo iwe ni yetu sote kwa kufurahia ukumbusho wa siku ya kuzaliwa kwako huku tukimshukuru Mungu kwa yote.
Wazazi na watoto wa mwisho ( Mapacha ) |
Familia. |
HAPPY BIRTHDAY MAMA.
Tuesday, November 1, 2011
Misaada na laana.
Kusaidiana siku zote ni kitu cha muhimu hasa pale unapokuwa unauhitaji kwani ni malengo tu ya kujaribu kuyafikia na kuyapunguza mahitaji yako ambayo kwa namna moja ama nyingine yana umuhimu katika kile kinachohitajika kufanyika .Suala langu katika hili leo ni kutaka kuongelea hasa suala la nchi hizi zilizoendelea ambazo ndizo mchango mkubwa sana wa nchi hizi zinazoendelea katika misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikipokelewa siku zote na imesaidia katika nyanja mbalimbali japo hii misaada huja na masharti ambayo kwa upande mwingine huonekana kama kutunyonya sana na kuwafaidisha sana hawa watoaji misaada. Katika hili leo nimesikia habari kutoka kwa waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon akisema ya kuwa ndoa za jinsia moja zinastahili kuhalalishwa na angalizo hatari ni pale anaposema kuwa kwa zile nchi zinazopokea misaada kutoka katika nchi hiyo zinapaswa kuafikiana na hilo jambo ama sivyo misaada itasitishwa katika nchi husika. Sawa una uwezo na wengi wanakutegemea katika mambo mengi tu ila swali ni je kwakuwa unategemewa na wengi au hata wachache ndio kisa cha kuwafanya wafanye au washabikie hata mambo ambayo kwa wengine ni kukaidi uhalisia wa maisha yao na hata kumkaidi Mungu? Inauma na kusikitisha sana na hapo naoana kama mwisho wa dunia kuelekea kwani hili suala sio la kawaida. Tusimkufuru Mungu hata kama tumejaliwa kuwa navyo jamani.
Thursday, October 27, 2011
Nawakumbuka marafiki zangu.
Kutoka kushoto, Mimi, Michael, Said na Emmanuel katika moja ya hafla tulipokuwa chuoni (May 2011) |
Ni wakati mwingi sana tulikuwa pamoja katika kufanikisha lengo letu la kisomo cha elimu ya juu pale chuoni. Hakika ni suala jema hasa pale tulipomaliza salama ila ilikuwa ni sala zaidi kwa kuwa Mungu alikuwa pamoja nasi katika kipindi kile chote na hata ushirikiano tulioonyesha baina yetu kama ndugu na naamini tumejenga undugu mzuri tu ambao utadumu daima na Mungu atutangulie katika lyote hasa katika ngwe hii mpya ya maisha.
Kaka Michael Filbert, Emmanuel Kasenga , Said Bakema, Fidelis Choga kiukweli mmekuwa chachu kubwa na nimejifunza mengi kupitia kwenu na hayo naamini nitayafanyia kazi na kuyaendeleza popote pale nitakapokuwa. Pia nawashukuru hata marafiki zangu wapendwa wengi tu japo siwezi kuwataja wote ila ni pamoja na France, Maiko, Said Kingu, Abraham, Willy, Pius, Stanley, Samwel, Gidion, Janeth, Leticia, Ramla, Rachel, Teddy, Debora, Emmy, Naumi, Noela, Tunsume, Julie, na wengineo wengi sana na bila kusahau makundi mbalimbali niliyofanikisha kufanya nayo mijadala mbalimbali juu ya masomo. I do remember you and i love u so so much and keep intouch . Much blessings and all the best.
Sunday, October 23, 2011
MICHEZO WIKIENDI.
HAPA NYUMBANI.
Hapa nyumbani tambo za kuutafuta ubingwa wa ligi kuu bado zinaendelea kwa timu kadhaa kuzidi kutafuta nafasi ya kuwa mabingwa japo bado imeonekana dhahili kuwa ni timu ya Simba na Yanga ndizo zinazidi kujikita kileleni baada ya zote kupata ushindi wikiendi hii na kuzifanya kuwa katika hali nzuri zaidi hasa katika kipindi hiki zinapotegemewa kukutana katika mpambano wa kukatana shoka wikiendi ijayo katika mchezo wa ligi.Simba iliyocheza na JKT Ruvu ilishinda 2-0 wakati mahasimu wao nao waliweza kushinda 1-0 dhidi ya JKT Oljoro.
NJE YA NCHI.
UINGEREZA.
Ligi mbalimbali pia ziliendelea katika nchi za nje ambapo nchini Uingereza matokeo ya kushangaza yalikuwa ni kati ya mahasimu Manchester United na Manchester City waliokipiga katika uwanja wa Old Trafford ambapo ilishuhudiwaMan Utd akilala nyumbani kwa mabao 6-1.Lawama za kichapo hicho dhahiri zitamwendea mlinzi wa Utd Evans aliyemtendea makosa mchezaji wa Man City Mario Balotelli na kuzawadiwa kadi nyekundu mapema katika kipindi cha pili.Matokeo mengine ya ligi ya English Premier League yalikuwa km ifuatavyo;
QPR 1- 0CHELSEA
ARSENAL 3- 1STOKE CITY
FULHAM 1- 3 EVERTON
LIVERPOOL 1- 1NORWICH CITY
HISPANIA.
MALAGA 0- 4 REAL MADRID
BARCELONA 0-0 SEVILLA
VALENCIA 1-1 BILBAO.
Sunday, October 16, 2011
Siku ya shukrani kwa familia yetu.
Tunamshukuru Mungu mweza wa yote kwa kuzidi kutulinda na kutujalia kile tunachomwomba katika maisha yetu.Tunasema asante na tunaomba uzidi kutufanikisha hata katika mahitaji yetu ya kila siku tuyaombayo kwani wewe ndiwe mpaji wa kila kitu maishani mwetu. Ni siku nyingine tumekuwa na furaha tele tulipoweza kujumuika na ndugu, jamaa na marafiki katika kutoa shukrani zetu kwa Mungu kwa yote aliyotutendea ambapo tulitoa shukrani zetu katika kanisa la kilutheri la mtaa wa Kagondo usharika wa Ibura pia na hafla ndogo ya kuwakaribisha wapendwa wetu Mama Paulina na Paulina pamoja na kutupongeza kwa kumaliza masomo ya chuo iliyofannyika katika ukumbi wa Bukoba club.Tunapenda kuwashukuru kwa uwepo wenu katika yote na Mungu awazidishie mema na moyo huo huo siku zote kwani undugu siku zote hujengwa na mengi.Pia tunawashukuru ndugu jamaa na marafiki walio mbali nasi kwa maombi yenu kufanikisha siku hii ya leo.Mungu awabariki.
Hapa ni wakati wa kutoa shukrani kanisani. |
Ndugu, jamaa na marafiki tuliosherehekea nao siku yetu. |
Saturday, October 15, 2011
Asante Mungu.
Ni vyema kumshukuru Mungu kwa kila jambo na hii haijalishi ni wakati gani bali ni muda wote ule na katika hali yoyote ile hivyo hata uwepo wangu katika blog hii ni kuzidi kumshukuru Mungu kwani nazidi kujifunza na kuyajua mengi kupitia kwa watu mbalimbali ambao wamekuwa na ujuzi na haya mambo nao ni pamoja na wapendwa kaka zangu Mubelwa na Alindwa Bandio pamoja na wengineo wengi ninaopitia kuzisoma blog zao hivyo nazidi kusema asante kwa hilo. Zaidi na zaidi napenda kutoa shukrani zangu kwa familia yangu Baba,Mama,Dadaz na ndugu jamaa na marafiki kwani bila nyie najua nisingeweza kufanya na kukutana na changamoto km hizi. La msingi ni kuzidi kutiana moyo ktk kuimarika hasa katika hiki nilichopendezwa nacho. Mungu awabariki.
Subscribe to:
Posts (Atom)