Thursday, November 17, 2011

HAPPY BIRTHDAY MARTIN. ( 18 NOV )



Katika kuikumbuka siku yako ya kuzaliwa leo tunakutakia kila la kheri na Mungu akujalie maisha marefu yenye AMANI, UPENDO na kila aina ya FANAKA.

HAPPY   BIRTHDAY  MARTIN.

Wednesday, November 16, 2011

HAPPY BIRTHDAY MAMA ( 17 Nov )

   
Dear  Mama.   

Mama  hongera  sana kwa  kuifikia  siku  ya leo ambayo   unakumbuka  siku ya  kuzaliwa kwako.  Awali  ya  yote  tunamshukuru  sana  Mwenyezi  Mungu  kwa  kukuzidishia  kila lililo  jema  na  hasa   afya  iliyo njema   ya  kukufikisha   siku  ya  leo.Tunajivunia  sana  kuwa  na wewe  Mama   kwani  kwa  pamoja  na  Baba  mmeweza  kutukuza  katika  malezi  yaliyo  bora  na  hata  kututimizia  kila  lililo  hitaji  katika  maisha  yetu  mpaka  leo.Mungu  awabariki  na kuwazidishia   na  naamini  kabisa  kwa  pale  milipopungukiwa  kwa kutuhangaikia  wanenu  Mungu atapajaza  tu. Mama  tunakushukuru  sana  kwa yote  na   tunazidi  kukuombea  kwa  Mwenyezi   Mungu  akuzidishia   siku  kama  hii  ya  leo  nyingi  tu  huko  mbeleni  na   naamini  tutazidi  tu kuikumbuka  siku  hii na kuiheshimu  siku zote.Umetufunza   mengi  na  umetukanya  mengi  ambayo leo hii  tunajivunia  na  kuyatambua.Hakika  hakuna  kama  Mama. Tunakupenda  sana  Mama  na   tunakuhitaji  sana  Mama  hivyo  tunaomba  hata siku  hii ya leo  iwe  ni  yetu  sote  kwa  kufurahia  ukumbusho  wa  siku  ya  kuzaliwa  kwako  huku  tukimshukuru  Mungu  kwa   yote. 

Wazazi  na watoto wa mwisho (  Mapacha )








Familia.
Kwa  pamoja tunayo  furaha kubwa sana kukutakia  kila   la kheri   na  uwe  na  siku  njema  Mama.

HAPPY          BIRTHDAY           MAMA.

Tuesday, November 1, 2011

Misaada na laana.


Kusaidiana  siku  zote  ni  kitu  cha  muhimu  hasa  pale  unapokuwa  unauhitaji  kwani  ni malengo tu ya  kujaribu  kuyafikia  na  kuyapunguza  mahitaji  yako  ambayo  kwa  namna  moja  ama  nyingine  yana umuhimu katika  kile kinachohitajika  kufanyika .Suala  langu  katika hili leo ni kutaka kuongelea  hasa suala  la nchi  hizi  zilizoendelea ambazo ndizo mchango  mkubwa  sana wa  nchi  hizi zinazoendelea katika  misaada  mbalimbali  ambayo imekuwa  ikipokelewa  siku zote  na  imesaidia  katika  nyanja  mbalimbali   japo hii  misaada huja  na  masharti   ambayo kwa upande mwingine  huonekana  kama kutunyonya sana na  kuwafaidisha  sana hawa  watoaji  misaada. Katika  hili leo nimesikia  habari   kutoka kwa  waziri  mkuu wa  Uingereza David  Cameroon akisema ya kuwa  ndoa  za jinsia  moja zinastahili kuhalalishwa  na  angalizo hatari ni pale  anaposema  kuwa kwa zile  nchi  zinazopokea misaada  kutoka  katika nchi  hiyo zinapaswa  kuafikiana  na hilo jambo  ama  sivyo  misaada  itasitishwa  katika nchi husika. Sawa  una  uwezo  na wengi wanakutegemea  katika  mambo mengi  tu ila swali ni  je  kwakuwa  unategemewa  na  wengi au hata  wachache ndio  kisa  cha kuwafanya wafanye au washabikie  hata mambo ambayo  kwa wengine ni  kukaidi uhalisia wa maisha yao na hata kumkaidi  Mungu?  Inauma na kusikitisha  sana na  hapo  naoana kama mwisho  wa dunia kuelekea  kwani hili suala sio  la  kawaida.  Tusimkufuru  Mungu  hata kama tumejaliwa kuwa navyo jamani.

Thursday, October 27, 2011

Nawakumbuka marafiki zangu.

Kutoka  kushoto, Mimi,  Michael,  Said  na Emmanuel katika moja ya hafla tulipokuwa chuoni (May 2011)






Ni   wakati   mwingi   sana  tulikuwa  pamoja katika kufanikisha lengo letu la kisomo cha elimu ya juu pale chuoni. Hakika ni suala jema hasa pale tulipomaliza  salama  ila  ilikuwa  ni  sala  zaidi  kwa   kuwa  Mungu alikuwa  pamoja  nasi  katika  kipindi  kile  chote  na  hata  ushirikiano  tulioonyesha  baina  yetu  kama ndugu na naamini  tumejenga  undugu mzuri  tu ambao  utadumu daima na Mungu atutangulie katika lyote  hasa katika ngwe  hii mpya  ya maisha.
Kaka  Michael  Filbert,  Emmanuel  Kasenga ,  Said  Bakema,  Fidelis  Choga  kiukweli mmekuwa chachu kubwa na nimejifunza mengi  kupitia  kwenu na  hayo naamini nitayafanyia kazi na kuyaendeleza   popote pale  nitakapokuwa. Pia nawashukuru hata marafiki zangu wapendwa wengi tu japo siwezi kuwataja wote ila  ni pamoja na France, Maiko, Said Kingu, Abraham, Willy, Pius, Stanley, Samwel, Gidion, Janeth, Leticia, Ramla, Rachel, Teddy, Debora, Emmy, Naumi, Noela, Tunsume, Julie, na  wengineo wengi sana  na bila kusahau makundi mbalimbali niliyofanikisha  kufanya nayo  mijadala mbalimbali  juu  ya  masomo.  I  do  remember you and  i  love u so so much and keep intouch . Much   blessings  and  all the  best.

Sunday, October 23, 2011

MICHEZO WIKIENDI.


 HAPA NYUMBANI.

Hapa nyumbani tambo za kuutafuta ubingwa wa ligi kuu bado zinaendelea kwa timu kadhaa kuzidi kutafuta nafasi ya kuwa mabingwa japo bado imeonekana dhahili kuwa ni timu ya Simba na Yanga ndizo zinazidi kujikita kileleni baada ya zote kupata ushindi wikiendi hii na kuzifanya kuwa katika hali nzuri zaidi hasa katika kipindi hiki zinapotegemewa kukutana katika mpambano wa kukatana shoka wikiendi ijayo katika mchezo wa ligi.Simba iliyocheza na JKT Ruvu ilishinda 2-0 wakati mahasimu wao nao waliweza kushinda 1-0 dhidi ya JKT Oljoro.

NJE   YA NCHI.

UINGEREZA.

Ligi mbalimbali pia ziliendelea katika nchi za nje ambapo nchini Uingereza matokeo ya kushangaza yalikuwa ni kati ya mahasimu Manchester United na Manchester City waliokipiga katika uwanja wa Old Trafford ambapo ilishuhudiwaMan Utd akilala nyumbani kwa mabao 6-1.Lawama za kichapo hicho dhahiri zitamwendea  mlinzi wa Utd Evans aliyemtendea makosa mchezaji wa Man City Mario Balotelli na kuzawadiwa kadi nyekundu mapema katika kipindi cha pili.Matokeo mengine ya ligi ya English Premier League yalikuwa km ifuatavyo;

QPR  1- 0CHELSEA 

ARSENAL 3- 1STOKE CITY 

FULHAM  1- 3 EVERTON  

LIVERPOOL  1- 1NORWICH CITY 


HISPANIA.

MALAGA  0- 4 REAL  MADRID

BARCELONA  0-0 SEVILLA

VALENCIA 1-1 BILBAO.

Sunday, October 16, 2011

Siku ya shukrani kwa familia yetu.




Tunamshukuru Mungu mweza wa yote kwa kuzidi kutulinda na kutujalia kile tunachomwomba katika maisha yetu.Tunasema asante na tunaomba uzidi  kutufanikisha hata katika mahitaji yetu ya kila siku tuyaombayo  kwani wewe ndiwe mpaji wa kila kitu maishani mwetu.  Ni siku nyingine tumekuwa na furaha tele tulipoweza kujumuika na ndugu, jamaa na marafiki katika kutoa shukrani zetu kwa Mungu kwa yote aliyotutendea  ambapo tulitoa shukrani zetu katika kanisa la kilutheri la mtaa wa Kagondo usharika wa Ibura pia na  hafla ndogo ya kuwakaribisha wapendwa wetu Mama Paulina na Paulina  pamoja na kutupongeza kwa kumaliza masomo ya chuo iliyofannyika katika ukumbi wa Bukoba club.Tunapenda  kuwashukuru kwa uwepo wenu katika yote na Mungu awazidishie mema na moyo huo huo siku zote kwani  undugu siku zote hujengwa na mengi.Pia tunawashukuru ndugu jamaa na marafiki walio mbali nasi kwa maombi yenu kufanikisha siku hii ya leo.Mungu awabariki.

Hapa ni wakati wa kutoa shukrani kanisani.










Ndugu, jamaa  na marafiki tuliosherehekea nao siku yetu.

Saturday, October 15, 2011

Asante Mungu.

Ni vyema kumshukuru Mungu kwa kila jambo na hii haijalishi ni wakati gani bali ni muda wote ule na katika hali yoyote ile hivyo hata uwepo wangu katika blog hii ni kuzidi kumshukuru Mungu kwani nazidi kujifunza na kuyajua mengi kupitia kwa watu mbalimbali ambao wamekuwa na ujuzi na haya mambo nao ni pamoja na wapendwa kaka zangu Mubelwa na Alindwa Bandio pamoja na wengineo wengi ninaopitia kuzisoma blog zao hivyo nazidi kusema asante kwa hilo. Zaidi na zaidi napenda kutoa shukrani zangu kwa familia yangu Baba,Mama,Dadaz na ndugu jamaa na marafiki kwani bila nyie najua nisingeweza kufanya na kukutana na changamoto km hizi. La msingi ni kuzidi kutiana moyo ktk kuimarika hasa katika hiki nilichopendezwa nacho. Mungu awabariki.