Monday, October 29, 2012

UKIMYA ULIOJAA MENGI YA KUSIMULIA MAISHANI.



Namshukuru  Mungu kwa kuzidi kuniweka hai na kuzidi kunipigania hata kuiona siku njema na kunijalia hata kuonekana kwa mara nyingine humu baada ya muda mrefu sana.Kiukweli ni ukimya  wa kipindi kirefu sana lakini ni ukimya ambao kiuhalisia una mambo mengi sana kutokana na mambo mbalimbali niliyoweza kupitia kwa kipindi cha miezi kadhaa. HAKIKA   TEMBEA   UONE    na ndivyo ilivyo mpaka sasa kwa upande wangu kwani nimepata fursa ya kujikita katika kazi ambayo kiukweli nimechanja sana mbuga na  kupajua hata nilipokuwa sitegemei kama ningeweza kufika kwa wakati mwafaka.Bado nachanja Mbuga na nitaandika mambo mbalimbali na mabandiko ya kusindikizia kile nikisemacho pale nitapojaliwa kumaliza  mzunguko huu.Much love.

Friday, April 20, 2012

Naikumbuka blog hii na sijaisusa.

Japo bado ni mwanzo tu katika kuangalia ni jinsi gani ninaweza kumudu na kuendeleza kusudi langu la kuwa katika himaya hii ya blog ila naamini palipo na kusudi na nia pia  basi mambo yatatengamaa.Naamini mmekuwa na mwanzo mwema wa mwaka  na mwendelezo mwema pia wa huu mwaka.Tuzidi tu kutakiana kila la kheri na tumtumainie yeye atutiaye  nguvu siku zote.

Wednesday, January 4, 2012

HAPPY BIRTHDAY DAD.

Dad,Mom na  Mapacha.



Tunamshukuru Mungu kwa kuzidi kutulinda na kuzidi kutukirimia afya iliyo njema.Na leo hii tunapokumbuka siku ya kuzaliwa kwako Baba yetu mpendwa tunazidi kukuombea maisha marefu yenye Amani,Upendo na kila aina ya Fanaka.Mungu akubariki nasi tuzidi kujifunza zaidi na zaidi kupitia kwako kama ilivyo kawaida yetu kupitia kwako.Tunakupenda sana Baba.