Tuesday, November 1, 2011

Misaada na laana.


Kusaidiana  siku  zote  ni  kitu  cha  muhimu  hasa  pale  unapokuwa  unauhitaji  kwani  ni malengo tu ya  kujaribu  kuyafikia  na  kuyapunguza  mahitaji  yako  ambayo  kwa  namna  moja  ama  nyingine  yana umuhimu katika  kile kinachohitajika  kufanyika .Suala  langu  katika hili leo ni kutaka kuongelea  hasa suala  la nchi  hizi  zilizoendelea ambazo ndizo mchango  mkubwa  sana wa  nchi  hizi zinazoendelea katika  misaada  mbalimbali  ambayo imekuwa  ikipokelewa  siku zote  na  imesaidia  katika  nyanja  mbalimbali   japo hii  misaada huja  na  masharti   ambayo kwa upande mwingine  huonekana  kama kutunyonya sana na  kuwafaidisha  sana hawa  watoaji  misaada. Katika  hili leo nimesikia  habari   kutoka kwa  waziri  mkuu wa  Uingereza David  Cameroon akisema ya kuwa  ndoa  za jinsia  moja zinastahili kuhalalishwa  na  angalizo hatari ni pale  anaposema  kuwa kwa zile  nchi  zinazopokea misaada  kutoka  katika nchi  hiyo zinapaswa  kuafikiana  na hilo jambo  ama  sivyo  misaada  itasitishwa  katika nchi husika. Sawa  una  uwezo  na wengi wanakutegemea  katika  mambo mengi  tu ila swali ni  je  kwakuwa  unategemewa  na  wengi au hata  wachache ndio  kisa  cha kuwafanya wafanye au washabikie  hata mambo ambayo  kwa wengine ni  kukaidi uhalisia wa maisha yao na hata kumkaidi  Mungu?  Inauma na kusikitisha  sana na  hapo  naoana kama mwisho  wa dunia kuelekea  kwani hili suala sio  la  kawaida.  Tusimkufuru  Mungu  hata kama tumejaliwa kuwa navyo jamani.

No comments:

Post a Comment