Saturday, October 15, 2011

Asante Mungu.

Ni vyema kumshukuru Mungu kwa kila jambo na hii haijalishi ni wakati gani bali ni muda wote ule na katika hali yoyote ile hivyo hata uwepo wangu katika blog hii ni kuzidi kumshukuru Mungu kwani nazidi kujifunza na kuyajua mengi kupitia kwa watu mbalimbali ambao wamekuwa na ujuzi na haya mambo nao ni pamoja na wapendwa kaka zangu Mubelwa na Alindwa Bandio pamoja na wengineo wengi ninaopitia kuzisoma blog zao hivyo nazidi kusema asante kwa hilo. Zaidi na zaidi napenda kutoa shukrani zangu kwa familia yangu Baba,Mama,Dadaz na ndugu jamaa na marafiki kwani bila nyie najua nisingeweza kufanya na kukutana na changamoto km hizi. La msingi ni kuzidi kutiana moyo ktk kuimarika hasa katika hiki nilichopendezwa nacho. Mungu awabariki.

No comments:

Post a Comment