Sunday, October 23, 2011

MICHEZO WIKIENDI.


 HAPA NYUMBANI.

Hapa nyumbani tambo za kuutafuta ubingwa wa ligi kuu bado zinaendelea kwa timu kadhaa kuzidi kutafuta nafasi ya kuwa mabingwa japo bado imeonekana dhahili kuwa ni timu ya Simba na Yanga ndizo zinazidi kujikita kileleni baada ya zote kupata ushindi wikiendi hii na kuzifanya kuwa katika hali nzuri zaidi hasa katika kipindi hiki zinapotegemewa kukutana katika mpambano wa kukatana shoka wikiendi ijayo katika mchezo wa ligi.Simba iliyocheza na JKT Ruvu ilishinda 2-0 wakati mahasimu wao nao waliweza kushinda 1-0 dhidi ya JKT Oljoro.

NJE   YA NCHI.

UINGEREZA.

Ligi mbalimbali pia ziliendelea katika nchi za nje ambapo nchini Uingereza matokeo ya kushangaza yalikuwa ni kati ya mahasimu Manchester United na Manchester City waliokipiga katika uwanja wa Old Trafford ambapo ilishuhudiwaMan Utd akilala nyumbani kwa mabao 6-1.Lawama za kichapo hicho dhahiri zitamwendea  mlinzi wa Utd Evans aliyemtendea makosa mchezaji wa Man City Mario Balotelli na kuzawadiwa kadi nyekundu mapema katika kipindi cha pili.Matokeo mengine ya ligi ya English Premier League yalikuwa km ifuatavyo;

QPR  1- 0CHELSEA 

ARSENAL 3- 1STOKE CITY 

FULHAM  1- 3 EVERTON  

LIVERPOOL  1- 1NORWICH CITY 


HISPANIA.

MALAGA  0- 4 REAL  MADRID

BARCELONA  0-0 SEVILLA

VALENCIA 1-1 BILBAO.

No comments:

Post a Comment