Wednesday, November 16, 2011

HAPPY BIRTHDAY MAMA ( 17 Nov )

   
Dear  Mama.   

Mama  hongera  sana kwa  kuifikia  siku  ya leo ambayo   unakumbuka  siku ya  kuzaliwa kwako.  Awali  ya  yote  tunamshukuru  sana  Mwenyezi  Mungu  kwa  kukuzidishia  kila lililo  jema  na  hasa   afya  iliyo njema   ya  kukufikisha   siku  ya  leo.Tunajivunia  sana  kuwa  na wewe  Mama   kwani  kwa  pamoja  na  Baba  mmeweza  kutukuza  katika  malezi  yaliyo  bora  na  hata  kututimizia  kila  lililo  hitaji  katika  maisha  yetu  mpaka  leo.Mungu  awabariki  na kuwazidishia   na  naamini  kabisa  kwa  pale  milipopungukiwa  kwa kutuhangaikia  wanenu  Mungu atapajaza  tu. Mama  tunakushukuru  sana  kwa yote  na   tunazidi  kukuombea  kwa  Mwenyezi   Mungu  akuzidishia   siku  kama  hii  ya  leo  nyingi  tu  huko  mbeleni  na   naamini  tutazidi  tu kuikumbuka  siku  hii na kuiheshimu  siku zote.Umetufunza   mengi  na  umetukanya  mengi  ambayo leo hii  tunajivunia  na  kuyatambua.Hakika  hakuna  kama  Mama. Tunakupenda  sana  Mama  na   tunakuhitaji  sana  Mama  hivyo  tunaomba  hata siku  hii ya leo  iwe  ni  yetu  sote  kwa  kufurahia  ukumbusho  wa  siku  ya  kuzaliwa  kwako  huku  tukimshukuru  Mungu  kwa   yote. 

Wazazi  na watoto wa mwisho (  Mapacha )








Familia.
Kwa  pamoja tunayo  furaha kubwa sana kukutakia  kila   la kheri   na  uwe  na  siku  njema  Mama.

HAPPY          BIRTHDAY           MAMA.

No comments:

Post a Comment